UMOJA NA MGAWANYIKO BIRA II-2012
Asalam aleykum wa ndugu zangu. Leo naja mezani tena kuuleta mjadala huu ambao umekuwa ukigonga vichwa vya wanafunzi kila kunapoitwa leo. Swali ni kwanini watu ndani ya BIRA II 2012 katika chuo chuo cha Ustawi Wa Jamii tuna mgawanyiko?
Jibu la swali hili haliitaji kuwaza sana. Kwa mtu mwenye upeo na uwezo wa kupambanua mambo atajua tatizo liko wapi hata kwa kuangalia mwenendo ndani ya darasa.
Nivyema kujua ya kuwa palipo na watu sitini kuna tabia sitini. Kisaikolojia watu hawafanani kuwaza, kunia na kuamua. Katika watu watu wote hao wapo wenye tabia nzuri na mbovu. Wapo wenye polojo wengine mnasema eti majungu, wambea, wapole na hata wale wengine!
Ni vigumu kujaribu kuunganisha watu wote hawa wakawa kitu kimoja. Jitihada zote utakazozifanya ni sawa na kujaribu kumvisha sketi mbuzi. Mbali na kuwa hana kiuno cha kuvaa sketi bado hata yeye haipendi sketi maana inamkera.
Darasa hili lina umoja ila lina watu wenye mtazamo tofauti. Hakika mtu hasiyependa majungu yaani polojo hawezi kamwe kuchangamana na kinara wa polojo. Japo wale wakali wa polojo wako tayari kuchangamana na yeyote katika kutafuta wapi atachota majungu.
Yaipovunjika makundi yetu ya hawali na kuundwa mapya yasiyokuwa rasimi eti ya kujadili ndipo mambo yalipoharibika. Watu tukayasaliti makundi yetu na kuunda makundi mapya tukikaribishana ki rafiki, kitabia na kimengine. Pale drsa zima lilipokuwa na makundi yasiyo zidi manne ndipo baraaa lilipoanza. Ikawa sio mijadala ya masomo bali kumjadili huyu na yule. Tabia hii ililifanya darasa kuwa na mgawanyiko mkubwa kati ya makundi yasipenda majungu na yale yanayotanguliza majungu kwenye kundi kama sala ya kufunguli majadiliano (discusion)
Kiukweli wale wasiopenda polojo ni wamoja pale drsani na wale wapenda polojo ni wamoja pale darasani. Sio swala la kushangaa kusikia mtu akisema mimi siwezi kwenda kudiskasi na watu fulani maana wao ni watu wa majungu! Sasa hapa kuna la kuangaika kumtafuta mchawi wa darasa? Wachawi ni sisi wenyewe. Amini ya kuwa mtu wa polojo anaweza kuugua asipopiga umbea siku nzima. Sasa itakuwa shughuli haya makundi kukaa pamoja kuutafuta mwafaka isipokuwa tu mchezo wa ushushushu ukome.
Binafsi sipendi majungu hata kidogo. Kwa maana hiyo sipendi hata kuchangamana na wao. Ila tufaamu ya kuwa polojo nyingine ni nzuri zile zinazodumisha urafiki na hutani lakini sio majungu. Katika suala la tabaka mbili kuu yaani wapenda majungu na wasiopenda ni vigumu darasa kuwa na umoja.
Muda mwingine huwa nawaza pasipo kuwa na majibu. Hivi labda mtu anaponyanyuka na kuanza kuponda wengine kuwa wana majungu hivi ajiwazia kwanza yeye na kujiweka katika hatua hipi? Wawezaje kuliona banzi katika jicho la mwenzio na ungali hujaliono boliti katika jicho lako? Hebu fikiri eti mtu anayesifika kwa polojo asimame na kupinga polojo! Badala ya watu kumsikiliza wataanza kunong'ona wakijiuliza iweje kinara wa polojo leo aseme tena polojo haifai? Ki ukweli badala ya kuwafikishia watu ujumbe utakuwa umeharibu kabisa. Hau ndio kusema shetani akizeeka ujigeuza Malaika?
Tuache hizo. Hapana mganga atakayekuja kutibu hili, dawa tunayo. Tuache polojo zisizokuwa za msingi
No comments:
Post a Comment