Wednesday, September 19, 2012

WALINDE WANAO DHIDI YA MITANDAO MIBOVU

Ukweli: Ingawa watoto wengi wanaopokea ujumbe wa kuwatongoza kwenye mtandao hupuuza au kufuta, unahitaji kuwaelimisha watoto wako kuhakikisha usalama wao.
v  Asilimia 42% ya watoto (umri 10-17) walikiri kuona picha za uchi kwenye mtandao, kwa mujibu wa uchunguzi wa 2005 wa Chuo kikuu cha New Hampshire.
v  Asilimia 66% ya watoto hao hawakufungua viunganishi walivyoviona au kutafuta viunganishi hivyo
v  Mtoto mmoja kati ya saba wenye umri baina ya 10-17 wametongozwa kwenye
mtandao.
v  Asilimia 43% ya utongozaji ulifanywa na watoto wengine chini ya umri wa miaka 18. Asilimia 11% kati ya utongozaji ulifanywa na watu ambao walifahamika tayari kwa walengwa.
  Walinde watoto wako kwa “kuonyesha” na “kuwaambia”

Kuonyesha:
v  Kama unawaruhusu watoto wako kutumia IM, vyumba vya mazungumzo, wasaidie kujiandikisha. Onyesha wasiyostahili kuandika, ili wasitoe habari zao za binafsi? Zungumzia juu ya aina ya mazungumzo yanafaa na yapi yasiyofaa.
    Hakikisha watoto wako wanatumia majina yasiyoelezea jinsia yao kwenye
  mtandao. Waonyeshe mifano ya majina kwenye mtandao ambayo hayafai ( kwa
  mfano: girliegr85 jinsia ya kike)
v  Waonyeshe watoto wako maelezo juu ya watoto wengine ambao wamekuwa
wahanga.
    Kuwaambia:
v  Waambie watoto wako wasijibu jumbe za kuwatongoza na kutoa habari kama kuna mtu anawafuata.
v  Waambie wasijibu barua pepe kutoka kwa watu wasiowafahamu. Ni sawa kutojibu kila barua pepe au mawasiliano.
v  Waambie watoto wasisambaze maelezo juu yao kukiwa pamoja na namba zao za simu na simu za mkononi, anwani, anwani pepe, majina yao kwenye mtandao, picha, shule na mji unakoishi. Eleza kwa nini hii ni ya hatari.
v  Eleza jinsi watu wanavyo”ongopa” kwenye mtandao. Waambie watoto wako kwamba kijana mwenye umri wa “miaka 16” anayetaka kukutana nawe huenda asiwe na umri huo. Anaweza kuwa mtu wa miaka 45 badala yake. Watu pia hudanganya kuwa wa jinsia tofauti kwenye mtandao. Unaweza kuwaonyesha watoto waliokomaa makala kuhusu waviziaji wa watoto wadogo kwenye mtandao wanaojaribu kukutana na watoto kwenyen mtandao kwa ajili ya ngono.
v  Waambie kamwe wasikutane na mtu yeyote ana kwa ana ambaye wamewasiliana kwenye mtandao. Huwezi kujua ni mtu wa aina gani
  (Personal Information) Maelezo ambayo wewe na wanao mnapaswa kuwa waangalifu juu yake kwenye mtandao, kama vile namba za simu za mkononi, barua pepe, jina unalotumia kwenye mtandao, jina la ukoo, anwani, na picha.

No comments:

Post a Comment