Sunday, May 27, 2012
MAVAZI NA UTAMADUNI WA MWAFRIKA
Nimerejea tena uwanjani. Ni katika kudadisi na kudadavua hili na lile. Leo ninalo suala moja tu nalo ni hili, "Lipi vazi linatufaa kama vazi la taifa".
Ninaposikia yakuwa kuna mpango wa watanzania kuletewa vazi la taifa ninapata shaka kiduchu! Hivi watanzania wa leo ususan vijana wanaotamani kutembea uchi wa mnyama barabarani watakubali kuvaa vazi hilo la taifa?
Kila nikijaribu kuwaza sana majibubu yanazidi kuwa mbali zaidi. Hivi utamaduni wa mwafrika tumeutupa wapi? Suala gani limezifanya mila zetu za zamani kufukiwa shimoni na kuiga yale ya wageni! Sisi mbona tunatia huruma jamani. Tunaukataa usisi na kuutukuza uwale! Huu ni upuuzi usiokuwa na msingi wowote.
Dada zetu nani amewaloga. Au msemo nyinyi ni maua nanyi mmesadiki. Kitu gani kinawafanya mtembee barabarani mkiwa uchi? Mbona mmesahau haya, au hamjui yakuwa nyinyi ni wazuri. Yaani mnapendeza hata msipojiremba. Sasa nyinyi badala ya kujilemba mnatembea uchi! Lo!
Mimi niseme hakuna mwanadamu aliyeumbwa na maungo ya kuvutia kama mwafrika (binti). Sasa kitu gani kiwafanye mjiuze miili yenu sokoni kama dagaa wa Kigoma wakati nyinyi ni lulu? Na hayo maziwa yenu mbona mnayafunga Tanganyika jeki nyinyi mnasema eti mna boost kidogo! Huu ni upuuzi kabisa. Wengine mnatumia dawa kuongeza ujazo wa maziwa yenu! Mmelogwa?
Yaani maziwa yakituna tena yakawa nje ndo mnapendeza? Hapo mmedanganywa mkadanganyika. Tena mnazo nguo mnaziita bluetooth. Yaani hizo mkivaa tunaona ama chup au tight. Iz it fair? Binti kupanda daladala watu uwape shida, ya nini?
Sasa kuna mtindo mpya. Eti mnasema taiti ndefu. Mwana dada kakupigia hiyo taiti ndefu na ki-topu. Ehh! Barabarani utadhani mwenda wazimu anapita!
Nanyinyi kaka zangu huu mtindo mmejifunza wapi? Hii nyinyi mnaiita kata kei. Sasa ndo kusema suruali haziwatoshi tena au ndo kutaka kurahisisha mambo? Mwanamume unamvutia nani na wewe? Umevaa nguo ya nje lakini chupi, boxer viko nje! Yaani kijana akiinama aibu. Sasa kama binti anafanya hivyo kutafuta soko wewe mwanamume unatafuta nini? Mimi nnavyo jua dume ndilo malanyingi linatongoza baada ya kuvutiwa! Sasa wewe na harakati za kutembea uchi mwanamume ni nini?
Ndugu zanguni tubadilike. Tusiyatupe maadili kwa kuiga mambo ya kigeni. Sawa hata mkitaka kujifunza baadhi angalia ni nini! Mbona hata mazuzu huchagua waokote nini jaani na sio kila kitu? Tubadilike; mabadiliko yanaanza na wewe. Fanya hivyo.
Jonas John R.
ISW
Monday, May 21, 2012
UMOJA NA MGAWANYIKO BIRA II-2012
Asalam aleykum wa ndugu zangu. Leo naja mezani tena kuuleta mjadala huu ambao umekuwa ukigonga vichwa vya wanafunzi kila kunapoitwa leo. Swali ni kwanini watu ndani ya BIRA II 2012 katika chuo chuo cha Ustawi Wa Jamii tuna mgawanyiko?
Jibu la swali hili haliitaji kuwaza sana. Kwa mtu mwenye upeo na uwezo wa kupambanua mambo atajua tatizo liko wapi hata kwa kuangalia mwenendo ndani ya darasa.
Nivyema kujua ya kuwa palipo na watu sitini kuna tabia sitini. Kisaikolojia watu hawafanani kuwaza, kunia na kuamua. Katika watu watu wote hao wapo wenye tabia nzuri na mbovu. Wapo wenye polojo wengine mnasema eti majungu, wambea, wapole na hata wale wengine!
Ni vigumu kujaribu kuunganisha watu wote hawa wakawa kitu kimoja. Jitihada zote utakazozifanya ni sawa na kujaribu kumvisha sketi mbuzi. Mbali na kuwa hana kiuno cha kuvaa sketi bado hata yeye haipendi sketi maana inamkera.
Darasa hili lina umoja ila lina watu wenye mtazamo tofauti. Hakika mtu hasiyependa majungu yaani polojo hawezi kamwe kuchangamana na kinara wa polojo. Japo wale wakali wa polojo wako tayari kuchangamana na yeyote katika kutafuta wapi atachota majungu.
Yaipovunjika makundi yetu ya hawali na kuundwa mapya yasiyokuwa rasimi eti ya kujadili ndipo mambo yalipoharibika. Watu tukayasaliti makundi yetu na kuunda makundi mapya tukikaribishana ki rafiki, kitabia na kimengine. Pale drsa zima lilipokuwa na makundi yasiyo zidi manne ndipo baraaa lilipoanza. Ikawa sio mijadala ya masomo bali kumjadili huyu na yule. Tabia hii ililifanya darasa kuwa na mgawanyiko mkubwa kati ya makundi yasipenda majungu na yale yanayotanguliza majungu kwenye kundi kama sala ya kufunguli majadiliano (discusion)
Kiukweli wale wasiopenda polojo ni wamoja pale drsani na wale wapenda polojo ni wamoja pale darasani. Sio swala la kushangaa kusikia mtu akisema mimi siwezi kwenda kudiskasi na watu fulani maana wao ni watu wa majungu! Sasa hapa kuna la kuangaika kumtafuta mchawi wa darasa? Wachawi ni sisi wenyewe. Amini ya kuwa mtu wa polojo anaweza kuugua asipopiga umbea siku nzima. Sasa itakuwa shughuli haya makundi kukaa pamoja kuutafuta mwafaka isipokuwa tu mchezo wa ushushushu ukome.
Binafsi sipendi majungu hata kidogo. Kwa maana hiyo sipendi hata kuchangamana na wao. Ila tufaamu ya kuwa polojo nyingine ni nzuri zile zinazodumisha urafiki na hutani lakini sio majungu. Katika suala la tabaka mbili kuu yaani wapenda majungu na wasiopenda ni vigumu darasa kuwa na umoja.
Muda mwingine huwa nawaza pasipo kuwa na majibu. Hivi labda mtu anaponyanyuka na kuanza kuponda wengine kuwa wana majungu hivi ajiwazia kwanza yeye na kujiweka katika hatua hipi? Wawezaje kuliona banzi katika jicho la mwenzio na ungali hujaliono boliti katika jicho lako? Hebu fikiri eti mtu anayesifika kwa polojo asimame na kupinga polojo! Badala ya watu kumsikiliza wataanza kunong'ona wakijiuliza iweje kinara wa polojo leo aseme tena polojo haifai? Ki ukweli badala ya kuwafikishia watu ujumbe utakuwa umeharibu kabisa. Hau ndio kusema shetani akizeeka ujigeuza Malaika?
Tuache hizo. Hapana mganga atakayekuja kutibu hili, dawa tunayo. Tuache polojo zisizokuwa za msingi
Asalam aleykum wa ndugu zangu. Leo naja mezani tena kuuleta mjadala huu ambao umekuwa ukigonga vichwa vya wanafunzi kila kunapoitwa leo. Swali ni kwanini watu ndani ya BIRA II 2012 katika chuo chuo cha Ustawi Wa Jamii tuna mgawanyiko?
Jibu la swali hili haliitaji kuwaza sana. Kwa mtu mwenye upeo na uwezo wa kupambanua mambo atajua tatizo liko wapi hata kwa kuangalia mwenendo ndani ya darasa.
Nivyema kujua ya kuwa palipo na watu sitini kuna tabia sitini. Kisaikolojia watu hawafanani kuwaza, kunia na kuamua. Katika watu watu wote hao wapo wenye tabia nzuri na mbovu. Wapo wenye polojo wengine mnasema eti majungu, wambea, wapole na hata wale wengine!
Ni vigumu kujaribu kuunganisha watu wote hawa wakawa kitu kimoja. Jitihada zote utakazozifanya ni sawa na kujaribu kumvisha sketi mbuzi. Mbali na kuwa hana kiuno cha kuvaa sketi bado hata yeye haipendi sketi maana inamkera.
Darasa hili lina umoja ila lina watu wenye mtazamo tofauti. Hakika mtu hasiyependa majungu yaani polojo hawezi kamwe kuchangamana na kinara wa polojo. Japo wale wakali wa polojo wako tayari kuchangamana na yeyote katika kutafuta wapi atachota majungu.
Yaipovunjika makundi yetu ya hawali na kuundwa mapya yasiyokuwa rasimi eti ya kujadili ndipo mambo yalipoharibika. Watu tukayasaliti makundi yetu na kuunda makundi mapya tukikaribishana ki rafiki, kitabia na kimengine. Pale drsa zima lilipokuwa na makundi yasiyo zidi manne ndipo baraaa lilipoanza. Ikawa sio mijadala ya masomo bali kumjadili huyu na yule. Tabia hii ililifanya darasa kuwa na mgawanyiko mkubwa kati ya makundi yasipenda majungu na yale yanayotanguliza majungu kwenye kundi kama sala ya kufunguli majadiliano (discusion)
Kiukweli wale wasiopenda polojo ni wamoja pale drsani na wale wapenda polojo ni wamoja pale darasani. Sio swala la kushangaa kusikia mtu akisema mimi siwezi kwenda kudiskasi na watu fulani maana wao ni watu wa majungu! Sasa hapa kuna la kuangaika kumtafuta mchawi wa darasa? Wachawi ni sisi wenyewe. Amini ya kuwa mtu wa polojo anaweza kuugua asipopiga umbea siku nzima. Sasa itakuwa shughuli haya makundi kukaa pamoja kuutafuta mwafaka isipokuwa tu mchezo wa ushushushu ukome.
Binafsi sipendi majungu hata kidogo. Kwa maana hiyo sipendi hata kuchangamana na wao. Ila tufaamu ya kuwa polojo nyingine ni nzuri zile zinazodumisha urafiki na hutani lakini sio majungu. Katika suala la tabaka mbili kuu yaani wapenda majungu na wasiopenda ni vigumu darasa kuwa na umoja.
Muda mwingine huwa nawaza pasipo kuwa na majibu. Hivi labda mtu anaponyanyuka na kuanza kuponda wengine kuwa wana majungu hivi ajiwazia kwanza yeye na kujiweka katika hatua hipi? Wawezaje kuliona banzi katika jicho la mwenzio na ungali hujaliono boliti katika jicho lako? Hebu fikiri eti mtu anayesifika kwa polojo asimame na kupinga polojo! Badala ya watu kumsikiliza wataanza kunong'ona wakijiuliza iweje kinara wa polojo leo aseme tena polojo haifai? Ki ukweli badala ya kuwafikishia watu ujumbe utakuwa umeharibu kabisa. Hau ndio kusema shetani akizeeka ujigeuza Malaika?
Tuache hizo. Hapana mganga atakayekuja kutibu hili, dawa tunayo. Tuache polojo zisizokuwa za msingi
Sunday, May 20, 2012
BODI YA MIKOPO NA USAJIRI MPYA!!!!!
Hule mfumo wa kujisajiri katika bodi ya mikopo kwa wanafunzi walioko vyuoni unendelea. Hakikisha unajisajiri sasa kupitia OLAS heslb. Ni muhimu kwako mwanafunzi uliyeko chuoni ususan mwaka wa tatu na wa nne. Do not miss. For more info fungua wavuti ya bodi ya mikopo
Thursday, May 17, 2012
TANZANIA NA RPM
Tanzania ni moja wapo ya nchi zinazoendelea. Hapana shaka ya kwamba katika kufikia miamoja utaanza na moja. Tangu tujipatie uhuru mwaka 1961, Tanzania imekuwa ikifanya jitihada za makusudi kuhakikisha maendeleo yanafikiwa kwa kutumia rasilimali zetu tulizo nazo.
Naamini kwa kiwango tulichofikia kinaelekea kutia moyo hususan kwa mwananchi anayeitakia maendeleo nchi hii. Kwa muda wa takriban miaka 50 ya uhuru, Tanzania imejitutumua na kujaribu kushughulika kwa sana kuwaletea wananchi maendeleo.
Tanzania ya sasa imejenga barabara nzuri za kusifika. Maeneo mengi ya nchi yetu sasa yanafikika ki urahisi kwa sababu ya ubora wa miundo mbinu tuliyonayo ususan barabara. Leo ni rahisi kwa mtu kusafiri kutoka Dar es salaam hadi kigoma kwa siku mbili tu mwendo wa basi. Tofauti na zamani ambapo ilikuwa ikimrazimu mtu kusafiri kwa takribani siku nne hadi tano kuitafuta Kigoma.
Dar es salaam hadi Mbeya kwetu wanasema 'kachwant'apasi'. Ninamaana gani? Leo waweza kutoka Dar kwenda kunywa chai Mbeya na kurudi Dar ukaendelea na zako shughuli. Vivyo hivyo hata kwenda kule kwetu Arusha na Kirimanjaro ni raha tupu! vijana wa leo wanasema ni kugusa tu..
Wasiwasi wangu ni utaratibu mzima ambao serikali imeuweka katika kuhakikisha inailinda miundombinu hiyo. Utaratibu wa kufanya ukarabati mara kwa mara (RPM) nchini ni duni sana. Miundo mbinu ya barabara inaligalimu taifa pesa nyingi sana. Ni haibu kwa nchi kama hii kuona kwamba inao uwezo wa kutoa pesa nyingi kutengeneza barabara ilihali inashindwa kuandaa bajeti ndogo tu ya ukarabati wa barabara zetu.
Usipoziba ufa gharama yake ni kujenga ukuta! Gharama za kujenga ukuta hamna, kwanini msizibe ufa? Viongozi serikalini hili hamlioni? Hau sio vipaumbele kwenu. Nasikitika sana ninapoiangalia barabara ya Mandela ya jijini Dar es salaam. Barabara imechoka sina hamu. Mitaro ya kupitishia maji imeharibika, maji yanaanza kuitafuna barabara. Sasa, nauliza, 'mnasubiri barabara ihishe muanze upya kujenga barabara? Au mnasubiri mradi uongezeke ili muombe pesa nyingi na nyingine mtie kapuni?
Inasikitisha, na inatia asira. Kushinda kufanya ukarabati mdogomdogo mpaka tatizo liwe kubwa ni wizi na ujambazi!
Tubadilike!!!!!
Tanzania ni moja wapo ya nchi zinazoendelea. Hapana shaka ya kwamba katika kufikia miamoja utaanza na moja. Tangu tujipatie uhuru mwaka 1961, Tanzania imekuwa ikifanya jitihada za makusudi kuhakikisha maendeleo yanafikiwa kwa kutumia rasilimali zetu tulizo nazo.
Naamini kwa kiwango tulichofikia kinaelekea kutia moyo hususan kwa mwananchi anayeitakia maendeleo nchi hii. Kwa muda wa takriban miaka 50 ya uhuru, Tanzania imejitutumua na kujaribu kushughulika kwa sana kuwaletea wananchi maendeleo.
Tanzania ya sasa imejenga barabara nzuri za kusifika. Maeneo mengi ya nchi yetu sasa yanafikika ki urahisi kwa sababu ya ubora wa miundo mbinu tuliyonayo ususan barabara. Leo ni rahisi kwa mtu kusafiri kutoka Dar es salaam hadi kigoma kwa siku mbili tu mwendo wa basi. Tofauti na zamani ambapo ilikuwa ikimrazimu mtu kusafiri kwa takribani siku nne hadi tano kuitafuta Kigoma.
Dar es salaam hadi Mbeya kwetu wanasema 'kachwant'apasi'. Ninamaana gani? Leo waweza kutoka Dar kwenda kunywa chai Mbeya na kurudi Dar ukaendelea na zako shughuli. Vivyo hivyo hata kwenda kule kwetu Arusha na Kirimanjaro ni raha tupu! vijana wa leo wanasema ni kugusa tu..
Wasiwasi wangu ni utaratibu mzima ambao serikali imeuweka katika kuhakikisha inailinda miundombinu hiyo. Utaratibu wa kufanya ukarabati mara kwa mara (RPM) nchini ni duni sana. Miundo mbinu ya barabara inaligalimu taifa pesa nyingi sana. Ni haibu kwa nchi kama hii kuona kwamba inao uwezo wa kutoa pesa nyingi kutengeneza barabara ilihali inashindwa kuandaa bajeti ndogo tu ya ukarabati wa barabara zetu.
Usipoziba ufa gharama yake ni kujenga ukuta! Gharama za kujenga ukuta hamna, kwanini msizibe ufa? Viongozi serikalini hili hamlioni? Hau sio vipaumbele kwenu. Nasikitika sana ninapoiangalia barabara ya Mandela ya jijini Dar es salaam. Barabara imechoka sina hamu. Mitaro ya kupitishia maji imeharibika, maji yanaanza kuitafuna barabara. Sasa, nauliza, 'mnasubiri barabara ihishe muanze upya kujenga barabara? Au mnasubiri mradi uongezeke ili muombe pesa nyingi na nyingine mtie kapuni?
Inasikitisha, na inatia asira. Kushinda kufanya ukarabati mdogomdogo mpaka tatizo liwe kubwa ni wizi na ujambazi!
Tubadilike!!!!!
Friday, May 11, 2012
HARAKATI HIZI, NINI MAANAYE?
Asalam aleykum wa ndugu zangu popote mlipo. nimatumaini yangu kuwa mu wazima wa afya. Leo nashika kalamu na karatasi tujadili hili....
Ni hivi karibuni katika chuo chetu cha Ustawi wa jamii tutakuwa na uchaguzi kumtafuta rais mpya chuoni kwetu. Wasiwasi wangu ni harakati za kashifa zinazojitokeza miongoni mwa tuliowengi. Nadhani tumesahau kosa la ushabiki tulilolifanya mwaka jana na kujipatia serikali zembe, hisiyo wajibika na hata hisiyokuwa na huruma kwa wanafunzi wake.
Kama kweli ingekuwa chama cha siasa kingekuwa ndicho kinachomuweka rais wa chuo madarakani basi tungekuwa na jibu moja yakuwa chama tawala hakirudi madarakani. Sasa sio hivyo, ni sera, uungwaji mkono na uwezo wako binafsi katika utendaji wa kazi.
Sio tu chama hicho kilichomuweka rais aliyepo madarakani kingepoteza kura mwaka huu bali hata ndani ya miaka mitatu kisingeweza kujitutumua kusimamisha mgombea kwa kile kilichoonekana kuwa ni udhaifu katika serikari hiyo.
Ndugu, kumpata kiongozi wa kukiongoza chuo sio sawa na kumtafuta kahaba wakati wa shida. Hapa ni vyema kumpima mgombea mwenyewe bila kusikiliza nani anasema nini. Ushabiki, chuki za ovyo zisizokuwa na maslai kwa chuo zisimfanye mtu ausaliti mwaka kwa kuweka pambo madarakani eti ni kiongozi.
Jpime, mpime mwenzio anayekurubuni. Jaribu kujua analolengo gani? Masuala binafsi ya mwenzio yasikupeleke ukaisahau misingi imara ya kumpata kiongozi imara. Watu wanasema dini, wanasema ukabila! Katika jamii za wasomi dini inamaana gani? Kabila lake linatuhusu nini sisi? Kwamba sawa anaweza kuongoza lakini tatizo ni dini yake! Haiji hata kidogo.
Watu wanaleta uchama uchama. Sisi chama cha mtu kinatuhusu nini? Kuna nini mpaka sisi tuanze kuangalia chama cha mtu? Hasa katika jamii ya watu wamoja wasiotengwa na siasa za vyama, kwao siasa za nini?
Kama maneno ya biblia yasemavyo, yatupasa tukumbuke wapi tulikojikwaa tukaanguka.
Jonas John
Asalam aleykum wa ndugu zangu popote mlipo. nimatumaini yangu kuwa mu wazima wa afya. Leo nashika kalamu na karatasi tujadili hili....
Ni hivi karibuni katika chuo chetu cha Ustawi wa jamii tutakuwa na uchaguzi kumtafuta rais mpya chuoni kwetu. Wasiwasi wangu ni harakati za kashifa zinazojitokeza miongoni mwa tuliowengi. Nadhani tumesahau kosa la ushabiki tulilolifanya mwaka jana na kujipatia serikali zembe, hisiyo wajibika na hata hisiyokuwa na huruma kwa wanafunzi wake.
Kama kweli ingekuwa chama cha siasa kingekuwa ndicho kinachomuweka rais wa chuo madarakani basi tungekuwa na jibu moja yakuwa chama tawala hakirudi madarakani. Sasa sio hivyo, ni sera, uungwaji mkono na uwezo wako binafsi katika utendaji wa kazi.
Sio tu chama hicho kilichomuweka rais aliyepo madarakani kingepoteza kura mwaka huu bali hata ndani ya miaka mitatu kisingeweza kujitutumua kusimamisha mgombea kwa kile kilichoonekana kuwa ni udhaifu katika serikari hiyo.
Ndugu, kumpata kiongozi wa kukiongoza chuo sio sawa na kumtafuta kahaba wakati wa shida. Hapa ni vyema kumpima mgombea mwenyewe bila kusikiliza nani anasema nini. Ushabiki, chuki za ovyo zisizokuwa na maslai kwa chuo zisimfanye mtu ausaliti mwaka kwa kuweka pambo madarakani eti ni kiongozi.
Jpime, mpime mwenzio anayekurubuni. Jaribu kujua analolengo gani? Masuala binafsi ya mwenzio yasikupeleke ukaisahau misingi imara ya kumpata kiongozi imara. Watu wanasema dini, wanasema ukabila! Katika jamii za wasomi dini inamaana gani? Kabila lake linatuhusu nini sisi? Kwamba sawa anaweza kuongoza lakini tatizo ni dini yake! Haiji hata kidogo.
Watu wanaleta uchama uchama. Sisi chama cha mtu kinatuhusu nini? Kuna nini mpaka sisi tuanze kuangalia chama cha mtu? Hasa katika jamii ya watu wamoja wasiotengwa na siasa za vyama, kwao siasa za nini?
Kama maneno ya biblia yasemavyo, yatupasa tukumbuke wapi tulikojikwaa tukaanguka.
Jonas John
Wednesday, May 2, 2012
MPAKA LINI?
Nawaza najiwazia,
majibu katu kichwani sipati,
Demokrasia uhuni au mbinu kutuziba midomo,
Aliyeshinda kashindwa aliyeshindwa kashinda.
Mwaka umefika,
chaguzi tumefanya,
wahuni mezani mwakaa,
matokeo kuyaadaa.
Madaraka mwashika,
mwalewa utukufu,
jamii mwaitosa,
hapana watendea haki.
Jamii sasa wazinduka,
Mpango kuwadondosha,
Hilo mwalibaini,
kura mwazipora.
Janja ya nyani,
Hii mwafanya,
jamii itaja kasirika
Nchi mtakimbia.
Jonas John R
Nawaza najiwazia,
majibu katu kichwani sipati,
Demokrasia uhuni au mbinu kutuziba midomo,
Aliyeshinda kashindwa aliyeshindwa kashinda.
Mwaka umefika,
chaguzi tumefanya,
wahuni mezani mwakaa,
matokeo kuyaadaa.
Madaraka mwashika,
mwalewa utukufu,
jamii mwaitosa,
hapana watendea haki.
Jamii sasa wazinduka,
Mpango kuwadondosha,
Hilo mwalibaini,
kura mwazipora.
Janja ya nyani,
Hii mwafanya,
jamii itaja kasirika
Nchi mtakimbia.
Jonas John R
Karibuni tutafakari pamoja
Wadau,
Mambo vipi?
Mbele yenu ni blog mpya. Blogu ambayo imeanzishwa nami mahsusi iwe uwanja wa kutafakari hili na lile katika yale yatuzungukayo kwenye maisha na mahusiano yetu kiuchumi, kisiasa, kiutamaduni na kijamii kwa ujumla wake.
Kwa nini Tutafakari? Kwa nini blog hii iitwe Tutafakari? Ni kwa kuwa tunapaswa kutafakari, tena si kutafakari peke yake, bali kutafakari kwa kina, kutafakari kwa marefu na mapana juu ya haya mambo yote yatuzungukayo.
Tutafakari.
Tutafakari kwa kuwa tunapotafakari ni dhahiri tunajipa nafasi ya kutafuta majawabu juu ya kadhia zote kwenye maisha yetu. Tusipotafakari, tuna lipi tutakalojifunza? Tuna lipi tutakalolitumia kama njia sahihi ya kukabiliana na changamoto zinazotujia kila siku kwenye maisha yetu? La hasha. Tusipotafakari, tunajichimbia kaburi la ujinga na umasikini.
Tutafakari.
Hivyo hili ni jukwaa la kutafakari. Tujadili kwa kina juu ya mustakabali wa taifa letu.
Karibuni sana kwa mchango wa mawazo katika kutafakari.
Tutafakari. Tutafakari kwa pamoja.
Ahsanteni sana.
Jonas John,
Dar es Salaam, Tanzania.
Mambo vipi?
Mbele yenu ni blog mpya. Blogu ambayo imeanzishwa nami mahsusi iwe uwanja wa kutafakari hili na lile katika yale yatuzungukayo kwenye maisha na mahusiano yetu kiuchumi, kisiasa, kiutamaduni na kijamii kwa ujumla wake.
Kwa nini Tutafakari? Kwa nini blog hii iitwe Tutafakari? Ni kwa kuwa tunapaswa kutafakari, tena si kutafakari peke yake, bali kutafakari kwa kina, kutafakari kwa marefu na mapana juu ya haya mambo yote yatuzungukayo.
Tutafakari.
Tutafakari kwa kuwa tunapotafakari ni dhahiri tunajipa nafasi ya kutafuta majawabu juu ya kadhia zote kwenye maisha yetu. Tusipotafakari, tuna lipi tutakalojifunza? Tuna lipi tutakalolitumia kama njia sahihi ya kukabiliana na changamoto zinazotujia kila siku kwenye maisha yetu? La hasha. Tusipotafakari, tunajichimbia kaburi la ujinga na umasikini.
Tutafakari.
Hivyo hili ni jukwaa la kutafakari. Tujadili kwa kina juu ya mustakabali wa taifa letu.
Karibuni sana kwa mchango wa mawazo katika kutafakari.
Tutafakari. Tutafakari kwa pamoja.
Ahsanteni sana.
Jonas John,
Dar es Salaam, Tanzania.
Subscribe to:
Comments (Atom)