Thursday, June 6, 2013

PEPE BINTI MAYUNGA

U binti uliyeumbika, mfano hakunaga
Mtoto unachanua, mfano wa maua
Yako sura tamu, mfano wa asari
Njoo kwangu malkia, uponye wangu mtima.

Sio siri umeniteka, sina budi kukiri
Haraka moyo waupeleka, kwako sijihimu
Unapendeza unapendeka, nakiri hili bayana

Sifa zo zaimbwa, kote zimeenea
Jinsi ulivyoumbika, mfano hakunaga
Macho yako hata mdomo, hata kipofu avutiwa
Njoo kwangu malkia, uuponye wangu mtima.

Si mfupi mrefu, waswahili eti wastani
Si mnene si mwembamba, bao umewafunga
Uzuri wako wasambaa, kama moto nyikani
Kila mtu ajihisi bahati, kuzungumza na wewe

Nimezunguka bara, nikaenda kule zanzibar
Kote mezunguka, mikoa ishirini na saba
Bado namba moja, chati washikilia
Wanukia wavutia, kama nguva baharini

Kifua mbele tembea uzuri jivunia
Muumba kakutunuku kakidhi yako haja
Wavutia mfano twiga, mbugani manyara

Lakini kumbuka, majivuno ondoa
Kiburi si maungwana, wengine susia
Jifanye nao sawa, japo sio sawa
Njoo kwangu malkia, uuponye wangu mtima.

Pepe wewe Pendo, mtoto umebalikiwa
Umbo lako safi, kama malaika nasema
Umewatoa nishai, wengi macho juujuu
Njoo kwangu malkia, uuponye wangu mtima

Rangi yako kama dhahabu, unawaka kama lulu
Ngozi yako raini, kama mwana paa sikia
Mguu chupa ya bia, hakuna mpinzani najua
Njoo kwangu malkia, uuponye wangu mtima.

Mwenzio niko taabuni, kwa pendo lako tamu
Kila leo ni mpya, mautundu kukazia
Wanipa kila kitu, mfano wa mwana kwa mamaye
Kila nikuonapo mimi hoi, moyo waupeleka mchaka

Mimi nimeanza, wengine watakiri
Hata wasiokiri, wivu wawashika
Wewe ni namba moja, zaidi yako hakuna
U mkari, mzuri wavutia, kama wewe duniani hakuna

Mwisho namaliza, hili zingatia
Sura hapana tisha, tabia myenendo pia
Shika maadiri bora, vigezo vyote timiza
UISHI KWA PENDO DUNIA YA MOLA

1 comment: